Ahoji maharage kuwa
hatari kwa afya???
![]() |
Wali kwa nyama |
Wataalaamu wa ubora wa vyakula kupitia Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii wametakiwa kufanya utafiti makini kuhusu ubora wa vyakula kabla ya kutangaza madhara ili kuondokana na mkanganyiko katika jamii.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar (SMZ), Balozi
Seif Ali Idd alisema hayo wakati akihutubia kwenye Kilele cha Maonyesho
ya Wakulima (Nanenane) Viwanja vya Nzuguni Dodoma ambako yalifanyika
kitaifa.
Balozi Idd alisema taarifa za harakaharaka kuhusu
ubora wa vyakula zinawakanganya wananchi na kwamba lazima zifanyiwe
utafiti wa kutosha kabla ya kuzitangaza.
Alitoa mfano wa taarifa iliyowahi kutangaza kwamba
maharage ni hatari kwa afya ya binadamu, jambo ambalo alisema
analitilia shaka kutokana na ukweli kwamba chakula cha aina hiyo
kinaliwa na Watanzania wengi.
‘’Jamani maharage ni chakula kikuu kwa Watanzania
wote, hivyo msitangaze madhara kwa harakaharaka bali ufanyike utafiti wa
kutosha.
Kuhusu maonyesho wakulima, Balozi Idd aliwapongeza
wakulima nchini kwa kazi kubwa na kwamba Serikali itaendelea
kushirikiana na wakulima ili kukifanya kilimo kiwe na tija.
Awali, akizungumza machache kwenye hafla hiyo,
Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika Christopher Chiza aliwaonya
wauzaji wa mbegu feki nchini akisema Serikali imejipanga kuwadhibiti vya
kutosha.
Chiza alisema Serikali haitawavumilia hata kidogo
wauzaji mbegu bandia za mazao mbalimbali yakiwamo mahindi, pamba na hata
maharage na kwamba tayari wachache walishakamatwa na wanashughulikiwa.
Hata hivyo aliwataka wakulima kununua pembejeo
kwenye maduka yaliyosajiliwa pekee ili kuepuka utapeli huo ikiwa ni
pamoja na kuwa na uhakika.
No comments:
Post a Comment