Wednesday, 7 August 2013

Waziri wa Mambo ya Nchi







 Urais si kuandikwa

 sana gazetini

 
ujumbe umefika


Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe ametahadharisha wanaowania urais 2015 kwa kusema ushindi wa urais haupatikani kwa kuandikwa sana kwenye magazeti bali kura za wananchi ndizo zinazoamua.
Membe aliyasema hayo juzi usiku alipokuwa akizungumza kwenye Kipindi cha ‘Jenerali On Monday’ kinachorushwa hewani kila Jumatatu na Kituo cha Televisheni cha Channel Ten.
Waziri huyo alialikwa kuzungumzia uchaguzi wa Zimbabwe uliofanyika wiki iliyopita na ndiye aliyekuwa kiongozi wa waangalizi kutoka Jumuiya ya Ushirikiano wa Kusini mwa Afrika, (Sadc).
Katika uchaguzi huo, Rais Robert Mugabe alitetea nafasi yake kwa kuzoa kura 2,110,434 ambazo ni sawa na asilimia 61% ya jumla ya kura zote, huku Kiongozi wa MDC-T, Morgan Tsvangirai akiambulia 34%. Tayari Tsvangirai amepinga matokeo hayo.
Akizungumzia kushindwa kwa Tsvangirai, alisema: “Vyombo vya habari vilikuwa vinamkubali, alikuwa anaandikwa sana, alikuwa na mashabiki wengi kwelikweli  na alikuwa anajiamini...huyu alijiamini mno kushinda, lakini hatimaye alianguka na hakuamini.

Uchaguzi Zimbabwe
Akizungumzia utata wa uchaguzi wa Zimbabwe kuwa baadhi ya mataifa ya Magharibi, Marekani, Uingereza na Australia kusema haukuwa huru na haki, Membe alisema: “Nilikuwa na Kundi la waangalizi 600 wa Sadc, walifanya kazi nzuri na walihakikisha mambo yanakwenda vizuri.

Vikosi vya Tanzania DRC
Akizungumzia wanajeshi wa Tanzania wa kulinda amani kwenye Mji wa Goma, nchini Congo, chini ya Umoja wa Mataifa (Monusco), alisema vijana wanafanya kazi nzuri na wamefanikiwa kuwakimbiza waasi wa M23 kutoka kwenye mji wao.
“Kule kuna makundi mawili; walinzi wa amani ambao wanalindwa na kifungu cha sita na hawa hawapigani, wanailinda amani na wapo wanaopigania amani. UN wanasema kama amani haipo, itafutwe na kisha ilindwe, sasa hawa wako kwa kifungu cha saba.
Kuhusu uvumi wa kutekwa askari wa Tanzania na majeshi ya M23, Membe alikanusha na kusema: “Hizi habari si kweli kabisa. Hakuna kitu kama hicho kwani hawa wamekuwa wazuri kwa kupiga propaganda...hata pasipoti inayotajwa ni kuundaunda tu ikatiwa ufundi kwenye kompyuta,” alisema.

Uhusiano wa Tanzania na Rwanda
 Kuhusu uhusiano wa Tanzania na Rwanda, Membe alisema  uhusiano wa nchi hizo mbili, uko imara, haujatetereka na kwamba wako wachache wanaotaka kutuchonganisha.
“Kama alivyosema Rais Jakaya Kikwete, urafiki wa Tanzania na Rwanda uko imara na ninataka kusema Watanzania tuwe makini na watu wanaotaka kutuchonganisha.
“Urafiki wetu na Rwanda ni wa siku nyingi, tumefanya mengi kwa Rwanda, itakumbukwa pia tuliwahi kumtetea Kagame kupelekwa Ufaransa kutokana na madai ya kuhusika kwake na kifo cha aliyekuwa kiongozi wa nchi hiyo, Juvenal Habyarimana.

Dawa za kulevya
Akizungumzia kushamiri kwa dawa za kulevya, Membe alionyesha masikitiko yake kwa wanaojihusisha na kusema kuwa zinaharibu diplomasia ya Tanzania.
Membe ambaye alisema wanaotaka urais wapige vita dawa za kulevya, alisema Tanzania ina sura nzuri katika medani ya kimataifa, lakini tatizo la dawa za kulevya linatia doa

No comments:

Post a Comment