Dawa za Kulevya; Wasanii
wawakemea vijana wenzao
Siku za hivi karibuni kumekuwa na matukio yanayowahusisha wasanii na tuhuma za utumiaji na ubebaji wa dawa za kulevya , kitendo ambacho kinawashushia hadhi kwani si tu wanahatarisha maisha yao na watuamiaji lakini wanachafua jina la nchi.
Kuna baadhi ya wasanii kwa nia njema waliwahi 
kujitangaza na kuahidi kuacha ambao ni pamoja na Langa  Kileo ambaye 
alijitangaza kuwa anatumia na hadi anafikwa na umauti mwezi uliopita, 
alikuwa ameshaacha kutumia.
 Rehema Chalamila ‘Ray C’ ambaye hadi sasa 
anapambana na tatizo hilo ingawa amefanikiwa kwa kiasi fulani lakini 
matumizi ya dawa hizo yalimrudisha nyuma na kumfanya aanze upya akirudi 
kwenye tasnia ya muziki.
 Rehema Chalamila ‘Ray C’ ambaye hadi sasa 
anapambana na tatizo hilo ingawa amefanikiwa kwa kiasi fulani lakini 
matumizi ya dawa hizo yalimrudisha nyuma na kumfanya aanze upya akirudi 
kwenye tasnia ya muziki.
Msanii mwingine aliyekuwa akiunda kundi la Nako 2 
Nako Soldiers, Ibra Da Hustler, nae hivi karibuni ametangaza kuwa 
alikuwa anatumia  dawa za kulevya na sasa anapambana kuacha.
Msanii wa Ragga ambaye aliwahi kutamba mwanzoni mwa miaka ya 2000, Mark 2 B alitangaza kutumia na sasa anapambana kuacha.
Hao ni baadhi tu kuna wengi wanaofanya siri na 
kuna ambao wamepotea kabisa hata habari zao hazisikiki kutokana na 
matumizi ya dawa hizo.
Kama hiyo haitoshi kuna wanaodaiwa kubeba  na 
wanafanya hivyo kwa muda mrefu sasa, kitu ambacho kimekuwa kikiwakatisha
 tamaa hata wazazi wenye watoto wao ambao wanataka kuwa wanamuziki, 
wakiamini kuwa watajiingiza katika matumizi ya dawa au kusafirisha.
Starehe iliwatafuta baadhi ya wasanii na kutaka wazungumzie hali hiyo na nini mitazamo yao hasa ukizingatia hiyo ni ajira yao.
Mwasiti Almasi
Anasema wasanii waangalie nafasi yao katika jamii 
kabla ya kufanya vitu ambavyo vinawaweka katika hatari ya kupoteza 
heshima yao na mashabiki wao, ambao wengi wao hawapendi matumizi ya 
mihadarati na hata wakati mwingine pombe kupita kiasi.
Anasema kuwa matumizi au ubebaji wa dawa za 
kulevya unawashushia heshima yao, kuwafanya waonekane  wahuni na kuzidi 
kuleta ugumu katika kuifanya jamii iuchukulie muziki na sanaa kwa jumla 
kama kazi nyingine.
Anaongeza kuwa ni vyema Serikali nayo ikatilia 
mkazo suala la kuhakikisha kazi za wasanii zinakuwa na ulinzi, kwa maana
 ya kumnufaisha mwanamuziki au mwigizaji mwenyewe tofauti na sasa ambapo
 wasanii wanategemea shoo pekee.
Ommy Dimpoz
Hussein Machozi
Hassan Tx Moshi
“Sanaa ni ajira Serikali ilitambue hilo na isimamie kazi za 
wasanii ili kuwapa nafasi ya kufurahia matunda ya kazi zao, naamini 
likifanyika hili litapunguza hata wimbi la vijana kujihusisha na ubebaji
 na utumiaji wa dawa za kulevya kwa kuwa watakuwa wanakipata kile 
wanachokifanyia kazi,” anasema Mwasiti.
Ommy Dimpoz
Anasema kuwa ubebaji na utumiaji wa dawa za 
kulenya ni hatari kwa kuwa una athari kwa pande zote mtumiaji, jamii na 
hata mbebaji.
Anaonyesha mshangao wake kwa kusema kuwa kwa nini 
vijana wanapoteza muda kufanya yale ambayo mwisho wake siku zote huwa ni
 mabaya, aliongeza sanaa nchini japo siyo sana, lakini inalipa na kama 
watafanya kazi kwa bidii watapata mafanikio bila kutumiwa na vigogo wa 
dawa za kulevya kuwa ‘punda’ wa kubebea au watumiaji.
“Ninachokiona hapa ni ukosefu wa ajira kwa vijana 
ndiyo maana wanakaa vijiweni na kushauriana kutumia na hatimaye wanakuwa
 mateja au makontena ya kubebea, lakini vijana nao watambue uhuru 
hauuzwi hivyo wautumie vizuri kujiletea maendeleo na siyo matatizo,” 
anasema Dimpoz.
Hussein Machozi
Anaanza kwa kuwaasa wasanii wa rika zote kwa 
kusema kuwa wao ni kioo cha jamii ambacho kikichafuka na wanaokiangalia 
wanachafuka pia, ambapo wakichafuka kuna aina mbili za uchafu wa upande 
wao  kwa kuiga mabaya yao au kwa upande wa kuacha kutumia  kazi zao.
Anafafanua kuwa kukubali kuwa kontena au kutumia 
hakupunguzi matatizo waliyonayo, bali ni kuyaongeza ambapo mwisho wa 
siku watakaoumia ni wao.
“Siamini kama kuna wasanii wenye mtaji mkubwa wa 
kubeba dawa au kuuza bali wanatumika na vigogo ambao wanajulikana lakini
 wao hawapatwi na madhara kwa kuwa hawatumii wala hawabebi na wala 
hawawashirikishi watu wa karibu nao kwa kujua ni hatari , inabidi 
wasanii na vijana kwa jumla wawe macho,” anaasa Machozi.
Hassan Tx Moshi
Anasema ni kitu cha ajabu sana kumwona kijana ana 
nguvu na kipaji kujiingiza katika masuala haya ambayo mara zote yamekuwa
 ni mwisho wa maisha ya wahusika, ama wafe au kupotea kwenye sanaa 
kabisa.
Anaongeza kuwa kuna starehe nyingi za kufanya na 
kuna njia nyingi za kuwafanya waende nje kuliko kujiingiza kwenye 
ubebaji au utumiaji, kwa lengo la kujitajirisha huku wakijua wanaharibu 
maisha yao.
Siwema Mohamed ‘Shilole’
Jokate Mwegelo
“Tena afadhali nimepata nafasi ya kutoa dukuduku langu kwa 
wasanii wenzangu kukubali kuwa vifungashio vya matajiri wachache huku 
wakibaki kuwa masikini na kuwatajirisha wengine na wao kudhoofu,” 
anashangaa Moshi.
Aidha Moshi aliwataka wasanii wenzake kufanya kazi
 kwa bidii, bila kuingiza mambo ambayo yanawashushia hadhi yao na 
kubadilisha maisha yao kiafya kimaadili na kimtazamo.
Siwema Mohamed ‘Shilole’
 Anasema kuwa kukubali kubeba au kutumia 
wamejiweka katika wakati mgumu wanapokuwa na safari za nje ya nchi, 
kwani hawataaminika tena.
Anasema hakuna haja ya kuchungwa kila mmoja 
afahamu kuwa yeye ni nani na anatakiwa kuifanyia nini jamii, lakini siku
 zote lengo ni jema, kuwa itendee mema na si maovu kwa kuipotosha kwa 
namna yoyote ile.
“Tutapata shida tukitaka kusafiri kwani hakuna 
atakayekuwa na imani na sisi kutokana na kuvuma sana siku hizi, kuwa 
tunatumia au kutumiwa kubeba dawa na hivyo itakuwa ngumu kupita katika 
viwanja vya ndege vya ndani na nje kwa kuwa tutaonekana wahalifu,” 
anaasa Shilole.
Jokate Mwegelo
Anasema kuwa wasanii wasikubali kutumiwa kwa kuwa 
wanahatarisha maisha yao na jamaa zao pia, kwani kwa kubeba wanaleta 
sumu nyumbani kwa kutumia wanaweka sumu mwilini.
Anasema waache kutafuta fedha au maisha kwa njia za mkato, badala yake wafanye kazi na watapata wanachokitaka.
“Tatizo wasanii wanatamni vitu vya kwenye mitandao
 na kudhani ni rahisi kuwa navyo bila kujali hao walionavyo wamevipataje
 na kwa muda gani, wao wanataka kurahisisha na kuvipata matokeo yake 
wanajikuta mateja au wabebaji  hakuna mkato katika maisha wakaze buti 
watafanikiwa,” anasema Jokate.
Aidha Jokate anasema kuwa wanafanya kitu mwaka huu
 bila kujali miaka ijayo watataka kuwa nani na kwa kashfa kama hii, 
hawawezi kufikia malengo kwani jina likichafuka kulisafisha ni kazi.
“Huwezi jua siku za baadaye unataka kuwa nani 
lakini kwa kashfa kama hizi huwezi kufikia malengo yako, kwani ukifanya 
mazuri kusahaulika ni rahisi kuliko mabaya kila mmoja atakuwa 
anayakumbuka na hakuna atakayetaka kubeba lawama isiyomuhusu, watu 
watakutenga na kukukana kwa kila jambo,” anasema Jokate
No comments:
Post a Comment