Saturday, 27 July 2013

DK Bilali asema, mabadiliko tabianchi bado tatizo Afrika


DK Bilali asema, mabadiliko 

tabianchi bado tatizo Afrika

 



Arusha. Makamu wa Rais, Dk Mohamed Gharib Bilal amesema mabadiliko ya tabia ya nchi yameathiri kwa kiwango kikubwa makazi ya watu wanaoishi maeneo ya mijini hasa katika nchi za Kiafrika, hivyo juhudi za makusudi zinapaswa kuchukuliwa ili kukabiliana na athari hizo.
Akifungua mkutano wa kimataifa wa siku tatu jana jijini Arusha, unaojadili changamoto ya ongezeko la kasi ya idadi ya watu mijini na maendeleo Afrika unaosababishwa na mabadiliko ya tabianchi alisema mkutano huo utatoa ufumbuzi ambao utafanyiwa kazi kutokana miji mingi kuzalisha takataka kwa asilimia 80.
Dk Bilal alisema tangu kongamano la Habitat II mwaka 1996 majadiliano juu ya idadi kubwa ya watu kuhamia mijini imepitia kwenye mabadiliko mbalimbali, hivyo suala la mabadiliko ya tabianchi kuendelea kuwa ni changamoto kubwa kimataifa.

No comments:

Post a Comment