NASHANGAA MSHITAKIWA
KUFUTUWA DHAMANA
![]() |
SHERIA MSUMENO |
Msumi alikuwa akitoa ushahidi katika kesi ya
kupokea rushwa inayomkabili Hakimu Pamela Kalala, anayedaiwa kuomba na
kupokea rushwa kutoka kwa mke wa mmoja wa washtakiwa ambao alikuwa
akisikiliza kesi yao, Josephine Omar Wageb.
Akiongozwa na Wakili wa Serikali, Sophia Gula,
Msumi, alidai kuwa katika tarehe asiyoikumbuka Februari, mwaka jana,
alipokea maelekezo ya kushughulikia barua ya malalamiko dhidi ya Hakimu
Kalala.
Alidai kuwa maelekezo hayo yalitolewa na Mkurugenzi wa Mahakama za Wilaya hadi Mahakama ya Rufani.
Alidai kuwa maelekezo hayo yaliambatana na barua
iliyoandikwa na Josephine, akimlalamikia Hakimu Kalala kufuta dhamana ya
mumewe, na mazingira yasiyoridhisha ya uendeshaji wa shauri la mumewe.
Alidai kuwa aliitisha jalada la kesi hiyo namba
703 ya mwaka 2008 na kwamba baada ya kulipitia, pamoja na mambo mengine
alibaini kuwa mshtakiwa alifutiwa dhamana bila sababu.
Alidai kuwa baadaye alimwandikia Jaji Mfawidhi muhtasari na maoni yake kwa maelekezo zaidi.
Wakati akihojiwa na Wakili wa utetezi, Karoli
Muluge, Msajili Msumi alidai kuwa wakati wakiwa katika mchakato wa
kulishughulikia suala hilo, walisikia kuwa mshtakiwa alikuwa
ameshafunguliwa mashtaka ya rushwa.
Alisema hata hivyo Josephine hakumwambia kuwa mshtakiwa alipokea rushwa kutoka kwake.
Wakati akihojiwa na wakili mwingine wa utetezi,
Twaha Taslima, alidai kuwa kesi hiyo ilikuwa imefikia hatua ya mwisho na
kwamba ilikuwa imeahirishwa mara kadhaa kusomwa hukumu.
Alisisitiza kuwa hukumu ya kesi hiyo ilikuwa
haijawahi kusomwa ingawa ilionyesha kuwa washtakiwa walikuwa wametiwa
hatiani wakisubiri kusomewa adhabu.
Msajili Msomi alidai kuwa katika jalada hilo
kulikuwa na mkanganyiko mkubwa kiasi kwamba Jaji Mfawidhi Bethuel Mmila,
alikusudia kumwita mshtakiwa ili kupata ufafanuzi wa mkanganyiko huo.
Alibainisha kuwa mkanganyiko huo ulikuwa ni hukumu iliyoandikwa
kwa mkono ambayo ilionyesha kuwa washtakiwa walikuwa wametiwa hatiani na
tayari wakiwa wameshahukumiwa adhabu.
Alihitimisha kuwa Jaji Mfawidhi alipomuuliza
mshtakiwa sababu za kutokusoma hukumu hiyo, alichokijibu kilikuwa ni
tofauti na alichokiandika.
Shahidi Lyimo alidai kuwa alipokea barua ya
malalamiko dhidi ya mshtakiwa na kwamba alipomhoji, mshtakiwa alidai
kuwa alikuwa akimfutia dhamana kwa kuwa alikuwa ameshamtia hatiani.
No comments:
Post a Comment