Watoto kuzaliwa kwa wazazi watatu
si wawili Mmoja!!!!
Ni ugunduzi mpya ambao unatarajiwa kupata upinzani kutoka kwa watu mbalimbali duniani
Wakati njia ya uzazi kwa upandikizaji wa mbegu
ikiendelea kushamiri pia katika Tanzania, wanasayansi wameendelea
kuvumbua njia zaidi za uundaji wa watoto ambapo sasa mtoto anaweza
kuzaliwa na wazazi watatu.
Mbinu hiyo ya uzalishaji itatumia upandikizaji
(IVF) ambapo vinasaba vya wazazi watatu vitachanganywa pamoja na
kinasaba kimojawapo kitatumika kuharibu magonjwa ya kurithi.
Imeelezwa kuwa mtoto wa kwanza mwenye wazazi
watatu anaweza kuzaliwa mapema mwaka 2015 baada ya utafiti huo wa muda
mrefu kuonyesha mafanikio mwezi Juni mwaka huu.
Wanasayansi wa Uingereza huenda wakaifanya nchi
yao kuwa ya kwanza kukubali na kuunda sheria ya uundwaji wa watoto hao
wenye vinasaba vya wazazi watatu licha ya kuwepo kwa hofu ya watoto
watakaotengenezwa kama mtindo.
Mchakato huo wa uundaji wa watoto hao utajumuisha
kuweka vinasaba katika yai la mama na mayai mengine kutoka kwa
mwanamume mchangiaji ambapo mtoto atakayezaliwa atakuwa na wazazi wawili
wa kike na mmoja wa kiume.
Kiongozi mkuu wa uvumbuzi huu, Profesa Doug Turnbull anasema mbinu ya uzalishaji huo itafanyika kwa kuchukua yai kutoka kwa mama na yai, jingine toka kwa mwanamke, ambaye atakuwa ni mchangiaji (donor).
Anaongeza, mayai hayo yatachanganywa kabla ya
kuondoa kiinitete au nyukilia(muundo wa seli unaobeba taarifa za
urithi:vinasaba) kutoka yai la mama mchangiaji, kisha kuwekwa katika
nyuklia za mama asili pamoja na mbegu za baba, kisha kuchavushwa.
Profesa Malise Kaisi wa Chuo Kikuu cha Sayansi ya
Tiba Shirikishi Muhimbili (Muhas) ambaye ni Mtanzania wa kwanza
kuzalisha watoto kwa njia ya upandikizaji (IVF) anasema kwa Tanzania
bado tupo nyuma mno kwa utalaamu huo uliovumbuliwa hivi karibuni.
Kwanza, Profesa Kaisi anasema Tanzania bado haina
mtaalamu wa masuala ya urithi na upandikizaji(embrologyst) hivyo ina
safari ndefu kufika huko.
Anauelezea mchakato huo na kusema una nia ya
kuondoa maradhi ya urithi ambayo kwa kiasi kikubwa yanasababishwa na
seli za nyuklia kutoka kwa mama.
‘Yai la mama linachanganywa na yai la mwanamke
mwingine bila yeye kujua, pamoja na mbegu za baba, kisha anaundwa mtoto
ambaye hatarithi ugonjwa wowote toka kwa baba au kwa mama,” anasema
Profesa
Anaongeza kuwa kuna idadi kubwa ya watoto wanaorithi maradhi
kutoka kwa wazazi wao hivyo njia hiyo pengine itasaidia kuondoa tatizo
hilo.
Anaeleza kuwa, maradhi ya misuli, moyo, utumbo
yanarithiwa kwa kiasi kikubwa na kusababisha kizazi chenye watu wenye
ulemavu au vifo vya watoto.
“Kitu cha muhimu hapa ni kuwa, uundaji huu
utasaidia kuondoa kabisa maradhi yanayorithiwa katika ukoo,” anasema
Profesa Turnbull.
Dk Josh Noreh, Daktari Bingwa wa Masuala ya Uzazi
na Mmiliki wa Kituo cha Upandikizaji cha Kenya(KIVF) anasema anafahamu
kuwa mchakato huo bado haujakamilika bali upo katika majaribio ya
maabara bado.
“Ninajua kuwa upo uwezekano huo, lakini mimi bado sijaweza kufanya hivyo lakini nikifika Uingereza mwezi Oktoba, nitajifunza na nitajaribu hapa Kenya na Tanzania,”
anasema Dk Noreh.
Mganga Mkuu wa Serikali ya Uingereza, Profesa Dame
Davies anasema uvumbuzi huo una maana kubwa ya kuondoa uwezekano wa
mtoto kupata maradhi ya kurithi ambayo mara nyingi husababishwa na mtoto
kuzaliwa na wazazi wawili tu.
“Ni matokeo ya hali ya juu ambayo yatasaidia kwa kiasi kikubwa watoto wasirithi Maradhi kutoka ukoo,” alisema.
Profesa Davies, anasema madaktari nchini humo
sasa wameanza mchakato wa kutunga sera ya kuzalishwa kwa watoto hao,
kuichambua na kuunda muswada kisha ikiwezekana kuupeleka bungeni. “Kama
wabunge wataikubali sheria hiyo mwishoni mwa mwaka 2014, mtoto wa kwanza
anaweza kuzaliwa mwaka 2015 mwanzoni,” anasema Profesa Davies.
Ingawa asilimia 99.8 ya vinasaba ikiwa ni pamoja
na tabia zetu zinazoonekana zinarithiwa kutoka kwa baba na mama na
kuhifadhiwa katika seli za nyukilia, kijisehemu kidogo cha vinasaba
hivyo, huhifadhiwa katika nyumba ya kuzalisha nguvu za
seli(mitochondria) na hutoka kwa mama pekee.
Hivyo basi, urithi unaopatikana toka kwa mama,
unaoingia katika mitochondria, huathiri zaidi mtoto na ndiyo maana
wanasayansi wametafiti njia hii itakayotumia wazazi wawili wanawake na
mwanamume mmoja.
Watafiti hao walipewa kiasi cha dola milioni sita
katika kufanikisha utafiti huo ambao madhumuni yake makuu ni kuondoa
magonjwa ya urithi au yanayotokana na familia kwa watoto na kwa vizazi
na vizazi. Inatarajiwa kuwa kati ya watoto watano hadi kumi wenye afya
watazaliwa na wazazi watatu kila mwaka.
Mtoto mmoja kati ya 6,500 huzaliwa na maradhi ya
urithi ambayo mara nyingi huwa ni matatizo ya kuona, kusikia, moyo,
mapafu, ini na pumu hivyo njia hiyo itasaidia watoto wasipate maradhi
kutoka katika ukoo.
Dk David King, Mkurugenzi wa Usimamiaji wa Vinasaba vya Ubinaadamu, anasema mbinu ya uzalishaji wa aina hiyo haina umuhimu na si salama.
“Ninafurahia mchakato huu na ninahisi kuwa tutaokoa watoto
watano hadi kumi wasizaliwe na maradhi ya kurithi au vifo vya awali.
Hiyo itafanyika bila kubadilisha sura au tabia zao na itawasaidia zaidi
wagumba,” anasema Profesa Davies.
Dk David King, Mkurugenzi wa Usimamiaji wa Vinasaba vya Ubinaadamu, anasema mbinu ya uzalishaji wa aina hiyo haina umuhimu na si salama.
Hata hivyo, baadhi ya makundi ya haki za binadamu
na wenye imani kali, nchi za Ulaya wameupinga mchakato huo wakidai kuwa
unaondosha dhana ya kiasili ya uzazi.
No comments:
Post a Comment