Hii siyo dini wala
itikadi, ni uhalifu


ya watu wasiojulikana saa moja usiku, kuwashambuliwa kwa kuwamwagia tindikali raia wa Uingereza, Kate Gee na Kirstie Trup wote wakiwa na umri wa miaka 18.
Shambulizi hilo lilifanyika katika eneo la
Shangani katika Mji Mkongwe wa Zanzibar. Tukio hili ni mfululizo wa
matukio kadhaa ya watu kushambuliwa kwa kumwagiwa tindikali hapa
Zanzibar.
Baadhi ya matukio kwa mfano kumwagiwa tindikali
kwa Katibu wa Mufti wa Zanzibar, Sheikh Fadhil Suleiman Soraga na
kumwagiwa tindikali kwa aliyekuwa Mkurugenzi wa Baraza la Manispaa,
hatujapata kusikia kama kuna watu waliokamatwa na kufikishwa mahakamani.
Ni jambo la kusikitisha na linalovunja moyo kuona
kwamba nchi yetu iliyokuwa ikisifika kwa hali ya amani, utulivu na
ukarimu wa watu wake leo imekuwa midomoni katika vyombo vya habari vya
kimataifa kwamba watu wanashambuliwa kwa kumwagiwa tindikali.
Tukiwa raia wema tuungane kwa nguvu moja na
Serikali katika kuwatafuta na kuwafichua wote wanaohusika na
kushambuliwa kwa raia hao wa Uingereza na wengine ambao wamepatwa na
mikasa ya aina hiyo.
Tayari Serikali kupitia kwa Waziri wa Habari
Utamaduni Utalii na Michezo Zanzibar, Said Ali Mbarouk imeshatoa kauli
ya kuwaomba wananchi washirikiane na vyombo vya dola kuwafichua wahalifu
waliotenda tukio lile.
Tunafarijika kuona kwamba Serikali imeahidi siyo
tu kukomesha vitendo hivyo, pia kuanza kuratibu na kusimamia kwa makini
zaidi biashara ya tindikali kwa kutunga sheria itakayoweka masharti
maalumu.
Tukio hili linapaswa kutokuingiza hisia zozote
zaidi ya uhalifu, maana siyo dini wala siasa inayoeleza mtu au kikundi
cha watu kufanya vitendo vya kuvunja sheria kama kilichofanywa.
Zanzibar ni moja kati ya nchi zenye historia
kongwe ya uvumilivu wa kidini ambapo pia ina historia ndefu ya dini za
Uislamu na Ukristo. Hivyo ni suala lililowazi kuwa vitendo vya watu
kumwagiwa tindikali ni vya kihalifu na hakuna budi tuvikatae kwa nguvu
zote.
Zanzibar dini zote za Uislamu na Ukristo ziliingia
mapema katika eneo hili na hakukuwa na matatizo miongoni mwa wananchi
wake na pia utamaduni wa watu wa Zanzibar kwa karne nyingi ni wa
kuvumiliana katika kila jambo.
Msikiti wa Kizimkazi ni uthibitisho usio na shaka
kwamba katika kipindi cha mwisho wa karne ya 11 AD kuingia karne ya 12
AD Zanzibaar tayari ilikuwa na Waislamu wengi.
Hata hivyo, pengine walikuwepo watu ambao bado
hawakusilimu. Ushahidi uliokuwepo katika kisiwa kidogo cha Mtambwe Mkuu
Pemba umeonesha kuwa mnamo karne ya 11 AD kulikuwa na baadhi ya watu
waliozikwa ambao hawakuwa wa miji ya Afrika ya Mashariki, walikuwa ni
wafuasi wa madhehebu ya Sunii/Shafii.
Kule Pemba kuna mabaki ya msikiti wa kale unaokadiriwa kujengwa
mwaka 1300 AD karibu na Ras Mkumbuu. Wanazuoni mbalimbali wanasema
kwamba Uislamu ulikuwa unaenea kwa haraka zaidi katika maeneo ya Bahari
ya Hindi kunako karne ya 14.
Kwa mujibu wa maelezo ya historia ya dini ya
Kikristo Zanzibar iliyoandikwa na Dayosisi ya Kanisa la Kianglikana
Zanzibar ni kwamba Ukristo kwenye Visiwa vya Zanzibar kihistoria unaweza
kuzungumzwa tangu wavumbuzi wa Kireno wakiwa hapa, hata hivyo siyo
rahisi kupata moja kwa moja mlolongo unaoonyesha hiyo historia.
Katika Mji Mkongwe, mji wa miaka 500, kuna
makanisa mawili ya Kikristo, ambayo hayakujengwa mbali sana kutoka moja
hadi lingine. Makanisa haya; moja la Kianglikana na lingine la
Kikatoliki.
Huko Mbweni, nje kidogo ya Mji wa Unguja, kuna
kanisa pia la Kianglikana ambalo nalo ni miongoni mwa makanisa makongwe
hapa Zanzibar.
Dayosisi hiyo inasema badala ya kuangalia haya
makanisa kama ushahidi wa Ukristo mkongwe Zanzibar, ule ushahidi wa
majina ya Kireno kwenye makaburi na vielelezo vinginevyo vinaonyesha
kwamba Ukristo kwenye visiwa hivi ulikuwepo tangu enzi hizo za wavumbuzi
wa Kireno.
Zanzibar hakuna udini, hakuna matatizo miongoni
mwa waumini wa dini tofauti, Wazanzibari wote wanaishi kwa kuvumiliana,
kuheshimiana na kupendana.
Matukio ya kushambuliwa kwa risasi viongozi wa
kidini yanaitia doa nchi hii yenye historia ndefu ya uvumilivu wa kidini
miongoni mwa watu wake.
Mfalme ambaye kwa wakati huo alikuwa Seyyid Sayyid
Barghash bin Said Al-Busaid alivutiwa na aliamua kutoa saa kubwa, ili
kuupamba mnara wa kengele ambao uliwekwa pembe ya Kusini Magharibi ya
jengo la Kanisa la Anglikana Mkunazini, saa hiyo hadi hivi leo ipo.
Ushahidi mwingine ambao unathibitisha uvumilivu wa
kidini Zanzibar ni ule uamuzi wa Serikali ya Zanzibar ilipoamua kutoa
stempu mwaka 1963 kuadhimisha historia ndefu ya uvumilivu wa kidini
Zanzibar.
Picha zilizowekwa kwenye Stempu zilijumuisha
Kanisa Kuu la Mtakatifu Joseph, Kanisa Kuu la Kristo, Msikiti wa
Malindi, Msikiti wa Hujjatul Islam na Hekalu la Kihindi.
Kadhalika, katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
hatuna matatizo kati ya Waislamu na Wakristo na hali hiyo
inajidhihirisha katika maisha ya kila siku ya raia wa nchi hii.
Katika Tanzania, uvumilivu wa kidini unaweza
kuupata katika nyumba za kupanga, Wakristo wengi wamepanga kwenye nyumba
za Waislamu na Waislamu wengi pia wamepanga katika nyumba za Wakristo
Kwa upande wa ndoa ambalo ni suala nyeti sana hasa inapokuwa
mume ni dini nyingine na mke ni dini nyingine, lakini hilo katika nchi
yetu si tatizo kwani Wakristo na Waislamu wameoana.
Kwa mantiki hiyo, hakuna udini katika maisha ya
kawaida ya Mzanzibari wala Mtanzania. Hawa ni wahalifu wasakwe hadi
wakamatwe, ili Zanzibar iendelee kuwa salama kwa wakazi na watalii
wanaoitembelea.
No comments:
Post a Comment