Ni dalili ya afya au ugonjwa?
 
Katika baadhi ya jamii zetu nyingi hasa kutoka bara la Afrika, 
kumejengeka dhana kuwa kitambi /unene huashiria utajiri. Mila, imani na 
desturi hii kwa kiasi fulani huchangia watu kutozingatia kanuni na 
taratibu za lishe bora, pengine hii inatokana na mwamko  mdogo wa elimu 
ya afya jamii. 
 
 

Wakati hali ikiwa hivyo miongoni mwa watu toka 
bara letu la Afrika, kwa upande wa nchi zilizoendelea, watu huamini kuwa
 unene/kitambi ni dalili tosha ya ugonjwa. Siyo hivyo tu bali pia 
historia ya magonjwa katika fani ya elimu afya jamii inatueleza hivyo.
 
 Kuna unene wa aina kuu mbili, kwanza ni ule unaosababishwa na 
kutozingatia kanuni na taratibu za lishe bora / balance diet. Kwa mfano 
ulaji wa vyakula vyenye kiasi kikubwa cha mafuta na wanga, unywaji wa 
mara kwa mara wa pombe kama vile bia pamoja na kutofanya mazoezi ya 
mwili na viungo. Aina ya pili ya unene ni ule unaotokana na urithi japo 
kwenye mada hii msisitizo zaidi ni kwenye aina ya kwanza ya unene.
 
 Kuna matatizo mbali mbali yanayo ambatana na  unene/kitambi. Mosi, 
madhara ya kiafya kama vile ugonjwa wa moyo, shinikizo la damu, kisukari
 aina ya pili /diabetes type II. Pili, madhara ya kisaikolojia, hasa 
pale mtu anapojishuku kupoteza mvuto/ aesthetic beauty. Hali imeshamiri 
sana hasa katika nchi zilizoendelea ambapo watu huchukulia unene/kitambi
 kama  ulemavu fulani wa kimwili. 
 
 Pamoja na hayo, wakati 
mwingine tunafanya makosa kuwahukumu binadamu kulingana na mwonekano wa 
maumbile yao, kwani hakuna hata moja kati yetu anaweza kuingilia kazi ya
 uumbaji, ninasema hivi kwasababu hatuwezi kujua ni nini chanzo hasa 
ambacho kinapelekea mtu kuwa mnene au kuwa na kitambi. Kama nilivyosema 
awali,  kuna aina ya unene/kitambi kinachotokana au kusababishwa na 
urithi.
 
 Namna ya kukabiliana na matatizo yatokanayo na 
unene/kitambi, wakati watu katika mataifa yanayoendelea, hujikita zaidi 
kwenye matumizi ya magari hasa magari binafsi, kidogo hali ni tofauti 
katika nchi zilizoendelea ambapo msisizito kwao ni kwenaye matumizi ya 
usafiri wa umma, matumizi ya baiskeli na hata matembezi ya miguu kwa 
sehemu zinazofikika. Kwa hili wenzetu wa mataifa yaliyoendelea 
wamefanikiwa vya kutosha kwa kuwekeza na kutenganisha barabara za magari
 na zile za waendesha baiskeli na watembea kwa miguu.
 
 Mwisho, 
njia pekee ya kukabiliana na  changamoto hii ya unene/kitambi, ni kwa 
kuzingitia kanuni za lishe bora kwa kujisomea majarida yanayohusu elimu 
ya afya kwa jamii na kujijengea tabia ya kufanya mazoezi ya mwili na 
viungo. Muhimu kuliko yote, kama itawezekana ni kupunguza ulaji wa nyama
 choma na unywaji wa bia wa mara kwa mara.
 
 
Ni dalili ya afya au ugonjwa?
Katika baadhi ya jamii zetu nyingi hasa kutoka bara la Afrika, kumejengeka dhana kuwa kitambi /unene huashiria utajiri. Mila, imani na desturi hii kwa kiasi fulani huchangia watu kutozingatia kanuni na taratibu za lishe bora, pengine hii inatokana na mwamko mdogo wa elimu ya afya jamii.
Kuna unene wa aina kuu mbili, kwanza ni ule unaosababishwa na kutozingatia kanuni na taratibu za lishe bora / balance diet. Kwa mfano ulaji wa vyakula vyenye kiasi kikubwa cha mafuta na wanga, unywaji wa mara kwa mara wa pombe kama vile bia pamoja na kutofanya mazoezi ya mwili na viungo. Aina ya pili ya unene ni ule unaotokana na urithi japo kwenye mada hii msisitizo zaidi ni kwenye aina ya kwanza ya unene.
Kuna matatizo mbali mbali yanayo ambatana na unene/kitambi. Mosi, madhara ya kiafya kama vile ugonjwa wa moyo, shinikizo la damu, kisukari aina ya pili /diabetes type II. Pili, madhara ya kisaikolojia, hasa pale mtu anapojishuku kupoteza mvuto/ aesthetic beauty. Hali imeshamiri sana hasa katika nchi zilizoendelea ambapo watu huchukulia unene/kitambi kama ulemavu fulani wa kimwili.
Pamoja na hayo, wakati mwingine tunafanya makosa kuwahukumu binadamu kulingana na mwonekano wa maumbile yao, kwani hakuna hata moja kati yetu anaweza kuingilia kazi ya uumbaji, ninasema hivi kwasababu hatuwezi kujua ni nini chanzo hasa ambacho kinapelekea mtu kuwa mnene au kuwa na kitambi. Kama nilivyosema awali, kuna aina ya unene/kitambi kinachotokana au kusababishwa na urithi.
Namna ya kukabiliana na matatizo yatokanayo na unene/kitambi, wakati watu katika mataifa yanayoendelea, hujikita zaidi kwenye matumizi ya magari hasa magari binafsi, kidogo hali ni tofauti katika nchi zilizoendelea ambapo msisizito kwao ni kwenaye matumizi ya usafiri wa umma, matumizi ya baiskeli na hata matembezi ya miguu kwa sehemu zinazofikika. Kwa hili wenzetu wa mataifa yaliyoendelea wamefanikiwa vya kutosha kwa kuwekeza na kutenganisha barabara za magari na zile za waendesha baiskeli na watembea kwa miguu.
Mwisho, njia pekee ya kukabiliana na changamoto hii ya unene/kitambi, ni kwa kuzingitia kanuni za lishe bora kwa kujisomea majarida yanayohusu elimu ya afya kwa jamii na kujijengea tabia ya kufanya mazoezi ya mwili na viungo. Muhimu kuliko yote, kama itawezekana ni kupunguza ulaji wa nyama choma na unywaji wa bia wa mara kwa mara.

No comments:
Post a Comment