Mtihani wa Darasa la saba Watahiniwa wachanganya na maswali...
 
 
 mitihani darasa la Saba
 ni kizengu mkuti! 
 
   
    
     
 MBUNGE wa 
kuteuliwa, James Mbatia (NCCR-Mageuzi), ameibua madudu mapya katika 
sekta ya elimu, ambao umebaini kwamba kwenye mitihani ya majaribio ya 
darasa la saba, baadhi ya maswali ya kuchagua, hayakuwa na majibu.
MBUNGE wa 
kuteuliwa, James Mbatia (NCCR-Mageuzi), ameibua madudu mapya katika 
sekta ya elimu, ambao umebaini kwamba kwenye mitihani ya majaribio ya 
darasa la saba, baadhi ya maswali ya kuchagua, hayakuwa na majibu.
Mitihani hiyo ya 
majaribio ya programu maalum ya matokeo makubwa sasa, kwa mujibu wa 
Mbatia ilifanywa na wanafunzi wa darasa la saba hivi karibuni katika 
masomo ya Hisabati, Kiswahili na Kiingereza katika wilaya 40 nchini.
Katika uozo huo 
ambao ameutaja kama kuwakatisha tamaa wanafunzi katika somo la Hisabati,
 Mbatia alisema maswali sita yalibainishwa na wataalamu wa Hesabu kuwa 
hayana majibu huku swali moja likiwashinda maprofesa waliofanya mtihani huo.
Alisema katika swali moja, namba 33 walimu wa hisabati katika shule kubwa za msingi walishindwa kulifanya na baadaye kubainika kuwa ni swali la mwanafunzi anayechukua fani ya uhandisi katika vyuo vya elimu ya juu.
Mabatia alisema 
katika mitihani hiyo, kunamakosa mbalimbali ya lugha pamoja na usahihi 
wa masuala mbalimbali, ikiwemo programu hiyo kuainishwa kama matokeo 
makubwa sasa huku jina la wizara likiandikwa Wizara ya Elimu na Mafunzo 
ya Ufundi Stadi.
Alisema katika 
mtihani huo wa hisabati,ambao wanafunzi wa darasa la saba walitakiwa 
kufanya kwa saa mbili, mtaalamu wa aligebra aliufanya kwa saa 2:10 na 
profesa saa 2:03 huku yeye akifanya kwa saa 2:19.
“Matokeo haya ni 
kuwakatisha tamaa na kuwaua wanafunzi kabla ya kufanya mitihani, ni 
lazima hatua madhubuti zichukuliwe kuokoa mapigo haya ya moyo wa Taifa 
ambayo yakizimika, Taifa linakufa,” alisema.
Mbatia alitoa 
mapendekezo yake ili kuokoa janga hili la elimu ikiwa ni pamoja na 
kuundwa kwa Tume ya Kudumu ya Elimu, itakayoshughulikia kuhakikisha 
ubora wa elimu nchini. Tume hiyo kwa mujibu wa Mbatia, inatakiwa kuwa na
 mamlaka ya kuhakiki utendaji wa taasisi mbalimbali za elimu, ambazo 
hadi sasa zimeonekana kutotimiza vyema wajibu wake.
“Ninaamini 
kwamba,tume hiyo itakapoundwa itasaidia kubainisha wazi nini falsafa na 
malengo hasa ya utoaji wa elimu nchini, kulingana na wakati tulionao, 
jambo ambalo halitakuwa geni kwani katika uongozi wa awamu ya kwanza, 
kulitungwa falsafa na miongozo mbalimbali,”alisema
Alisema kwa 
mamlaka aliyonayo Rais na na kwa mujibu wa katiba na kwa kadri anavyoona
 inafaa, anaweza kuunda tume na kuipatia majukumu ya utendaji stahiki, 
ikiwemo kutoa idhini ya matumizi ya mitaala mingine.
Pia alipendekeza 
tume hiyo ihariri na kupitia vitabu vya kiada kwa shule nchini na 
kufanya utafiti za kisayansi kuhusu masuala mbalimbali ya elimu kwa 
lengo la kuinua ubora wa elimu.
Akizungumza na 
gazeti hili, Msemaji wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Bunyanzu 
Ntambi alikiri kuwa jinala wizara limekosewa katika mitihani hiyo. 
Alipoulizwa kuhusu uozo uliopo katika mitihani hiyo ya majaribio, 
alisema atafuatilia na atatoa taarifa kwa gazeti hili baadaye.
 
 
 
 
 
          
      
 
  
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment