- WACHUNGAJI WA DECI WAHUKUMIWA
 - WALIOPANDA MBEGU KURUDISHIWA 
 
|  | 
| Wana maombi | 
 
 
|  | 
| - WACHUNGAJI WA DECI WAHUKUMIWA | 
Vigogo wanne wa iliyokuwa Kampuni ya Development Entrepreneurship for 
Community Initiative (DECI) wamehukumiwa kwenda jela miaka mitatu au 
kulipa faini ya sh milioni 21 kila mmoja.
|  | 
| Wana maombi | 
 
 
Hukumu hiyo ilitokewa na Hakimu Mkazi Alocye Katemana wa Mahakama ya 
Kisutu, Dar es Salaam. Aidha, Mahakama imeagiza kuwa pamoja na adhabu 
hiyo Serikali ifanye mchanganuo wa mali za DECI ambazo inazishikilia, 
kwa kuwa zipo mali zilishikiliwa zisizo za kampuni hiyo bali za watu 
wengine.
 
 Alisema kuwa fedha za wateja wa DECI walizopanda 
zirejeshwe kwa wateja wenyewe ambao wataonesha uthibitisho wa kweli kuwa
 walipanda fedha zao huko.
 
 Katika hukumu hiyo iliyotolewa na 
Hakimu Mkazi, Stewart Sanga na kusomwa na Hakimu Katemana, washitakiwa 
walikuwa watano, ambao ni Jackson Mtares, Dominick Kigendi, Timotheo ole
 Loitginye, Samwel Mtares na Arbogast Kipilima. Hata hivyo Arbogast 
Kipilima aliachiliwa huru baada ya Mahakama kutokumpata na hatia.
 
 Washitakiwa hao walikuwa wanatetewa na mawakili wa kujitegemea Hudson Ndusyepo na Onesmo Kyauke.
 
 
 Wakili Mwangamila alidai washitakiwa hao wanakabiliwa na mashitaka 
mawili ambayo ni kuendesha na kusimamia mradi wa upatu kinyume cha 
kifungu 111A (1,3) cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu Sura ya 16.
 
 
Alidai kuwa, kati ya mwaka 2007 na Machi 2009, katika makao makuu ya 
DECI , yaliyopo Mabibo Mwisho, jijini Dar es Salaam, washitakiwa 
waliendesha na kusimamia mradi wa upatu katika sehemu tofauti nchini, 
kwa ahadi ya kuwapa wanachama wao fedha zaidi ambazo katika mazingira ya
 kibiashara ni kubwa kuliko mradi waliokuwa wakiufanya.
 
 
 
Mwangamila alidai kuwa, shitaka la pili ni kupokea amana za umma bila 
kuwa na leseni, kinyume cha kifungu cha 6 (1,2) cha Sheria ya mabenki na
 Taasisi za Fedha Na. 5 ya mwaka 2006 na kwamba, washitakiwa wote katika
 kipindi hicho wakiwa kwenye ofisi zao za DECI , walipokea amana kutoka 
kwa umma bila leseni.
|  | 
| Zigua simo na njero | 
 
 
No comments:
Post a Comment