Wednesday, 7 August 2013

waendesha pikipiki (bodaboda)


Bodaboda ni janga, 

Serikali Hili



Katika siku za hivi karibuni kumeibuka tabia ya waendesha pikipiki maarufu kama bodaboda kujichukulia sheria mkononi pindi kunapotokea ajali zinazohusisha magari na pikipiki.
wazi hilo
elimu kutolewa
Bila kujali ni nani mwenye makosa katika ajali hizi, waendesha pikipiki hao wameanzisha mtandao wa kuwashambulia madereva wa magari yanayohusika katika ajali hata kama wao ndio wenye makosa.
Mara tu ajali inapotokea, huanza kupigiana simu na kuitana na baada ya dakika chache utakuta kundi kubwa la waendesha bodaboda hao wamezingira gari na kuanza kujichukulia sheria mkononi.
Vijana hao badala ya kutoa taarifa polisi ili wafike na kufanya kazi yao, wao ndiyo hugeuka polisi na kuingia mitaani kumsaka aliyesababisha ajali iwapo anakuwa ametoweka kunusuru maisha yake.
Wanapomkuta “mhalifu”, badala ya kumpeleka polisi wao wanaamua kumsulubu kana kwamba wao wako juu ya sheria.
Kwenye gari lililohusika kwenye ajali, baadhi yao huvunja vioo, wengine hutembezea kipigo kwa dereva na hata abiria wasiohusika, kuiba mali za waliokuwepo kwenye gari husika na mara kadhaa imetokea hata kuchoma moto magari.
Tabia hii ikiachwa izoeleke kwamba bodaboda wajichukulie sheria mkononi, hakika tutakuwa tunatengeneza bomu la hatari.
Tayari kumeanza kujitokeza uhasama kati ya madereva wa magari na bodaboda kiasi kwamba wamiliki wa magari sasa hawataki kutoa msaada kwa waendesha bodaboda wanapopata ajali.
Nimeshuhudia mmoja amegongwa na kila gari lililokuwa linapita eneo la ajali dereva akiombwa msaada, utasikia “hao wamezidi”.
Asilimia 95 ya ajali zote zinazotokea nchini zikihusisha pikipiki, chanzo cha ajali hizo mara nyingi kinakuwa ni wenyewe waendesha pikipiki. Huu ndiyo ukweli, kwamba sasa hili ni janga la kitaifa.
Ni jambo la kawaida mwendesha bodaboda kulipita gari kupitia upande wa kushoto na wakati mwingine dereva wa gari ameshaonyesha ishara kuwa anakata upande wa kushoto. Wakati mwingine pikipiki mbili hulipita gari kwa wakati mmoja, kila moja ikipita upande wake.
Na si ajabu kukuta mwendesha bodaboda anawasha taa akionyesha ishara kuwa anakata kulia, lakini akakata kushoto au kinyume chake.


Katika siku za hivi karibuni kumeibuka tabia ya waendesha pikipiki maarufu kama bodaboda kujichukulia sheria mkononi pindi kunapotokea ajali zinazohusisha magari na pikipiki.
Bila kujali ni nani mwenye makosa katika ajali hizi, waendesha pikipiki hao wameanzisha mtandao wa kuwashambulia madereva wa magari yanayohusika katika ajali hata kama wao ndio wenye makosa.
Mara tu ajali inapotokea, huanza kupigiana simu na kuitana na baada ya dakika chache utakuta kundi kubwa la waendesha bodaboda hao wamezingira gari na kuanza kujichukulia sheria mkononi.
Vijana hao badala ya kutoa taarifa polisi ili wafike na kufanya kazi yao, wao ndiyo hugeuka polisi na kuingia mitaani kumsaka aliyesababisha ajali iwapo anakuwa ametoweka kunusuru maisha yake.
Wanapomkuta “mhalifu”, badala ya kumpeleka polisi wao wanaamua kumsulubu kana kwamba wao wako juu ya sheria.
Kwenye gari lililohusika kwenye ajali, baadhi yao huvunja vioo, wengine hutembezea kipigo kwa dereva na hata abiria wasiohusika, kuiba mali za waliokuwepo kwenye gari husika na mara kadhaa imetokea hata kuchoma moto magari.
Tabia hii ikiachwa izoeleke kwamba bodaboda wajichukulie sheria mkononi, hakika tutakuwa tunatengeneza bomu la hatari.
Tayari kumeanza kujitokeza uhasama kati ya madereva wa magari na bodaboda kiasi kwamba wamiliki wa magari sasa hawataki kutoa msaada kwa waendesha bodaboda wanapopata ajali.
Nimeshuhudia mmoja amegongwa na kila gari lililokuwa linapita eneo la ajali dereva akiombwa msaada, utasikia “hao wamezidi”.
Asilimia 95 ya ajali zote zinazotokea nchini zikihusisha pikipiki, chanzo cha ajali hizo mara nyingi kinakuwa ni wenyewe waendesha pikipiki. Huu ndiyo ukweli, kwamba sasa hili ni janga la kitaifa.
Ni jambo la kawaida mwendesha bodaboda kulipita gari kupitia upande wa kushoto na wakati mwingine dereva wa gari ameshaonyesha ishara kuwa anakata upande wa kushoto. Wakati mwingine pikipiki mbili hulipita gari kwa wakati mmoja, kila moja ikipita upande wake.
Na si ajabu kukuta mwendesha bodaboda anawasha taa akionyesha ishara kuwa anakata kulia, lakini akakata kushoto au kinyume chake.

No comments:

Post a Comment