Saturday, 20 July 2013

KITENGO CHA MAHELA....watu wataka kutoana vishipa..hahahahhaaahha!

 
 KITENGO CHA MAHELA
 
 
Leo nimesoma kuwa Kitengo cha Fedha  chatoa tamko kuhusu kodi ya laini ya simu aka sim card tax : 
"amewataka watumiaji wa mitandao ya simu nchini na watanzania kwa ujumla kuwa na subira kuhusu tozo ya Sh 1,000 kwa mwezi ..Alisema serikali inaendelea kupokea maoni kuhusiana na suala hilo .. tangu itolewe kauli hiyo yamekuwapo manung’uniko mengi kutoka kwa watu mbalimbali wakiwamo watumiaji wa mitandao ya simu" 
 
Sasa mi naomba tafadhali kama mwananchi na mpiga kura, viongozi wetu WASITUTANIE .. kodi au tozo hii kandamizi ilitungiwa kipengele katika sheria na ilipitishwa tena kinyemela bungeni.. sasa maoni wanachukua ya nini??!! Basi wasubiri mpaka warudi bungeni tutawapelekea salamu zao.
Ndugu zangu... wasituchanganye na tamko hili za kukinzana/kutuchanganya .........tetetetetetetetetete!!!!!!!!!!

No comments:

Post a Comment