Thursday, 18 July 2013

mtoto wa TANDALE

  1.  

     

      jamani hakuna mtu wa kumpa

     medali huyu jamaaa!!! 

     

    Kuna jamaa alikuwa anaishi karibu
    na makaburi. Basi akajigundulia njia
    ya kupata usafiri bila ya kulipa...
    Akawa kila akikodi bodaboda au
    bajaji mida ya jioni jioni alikuwa
    anaomba kuachwa makaburini.....
    Katikati ya safari akawa anajipaka
    poda usoni na kuweka pamba
    kwenye pua zake then wakati wa
    kushuka anaongea kwa kubana
    pua...

    .
    "Nimefika home unanidai shilingi
    ngapi?!?"
    .Madereva wote wa bodaboda na
    bajaji walikuwa wanatoka nduki....
    Siku moja akafanya mchezo huo
    kwa dereva mmoja wa bodaboda
    mtoto wa TANDALE kapinda
    mbaya!!! Walipofika mwisho wa
    safari dereva wa bodaboda
    hakutishika na mapoda wala pamba
    puani....

    Akakomaa anataka nauli
    yake!!!!
    JAMAA: "Ooooooky!!!! Twende
    kwenye kaburi langu nikakupe
    chako....!!!"
    Dereva ya boda boda kumbe
    alikuwa ameshaskia story za jamaa
    so akakomaa na kumwambia...
    BAJAJI: "Haina noma mtu wangu....
    Twende ukanipe changu nsepe...."

    maana hasira nilizonazo naweza kukulamba wewe na mapoda yako
    Walipofika kaburi fulani, jamaa
    akagonga msalaba....
    JAMAA: "Wakulu, wakulu fungueni
    nipeni alfu nane huyu jamaa
    ananidai nauli......!!!!"
    Ghafla mkono mrefu wenye
    manyoya ukatoka kaburini ukiwa
    umeshika noti ya msimbazi....

    DAAAH, NDUGU ZANGU ASUBUHI
    KULIKUTWA PEA MBILI TUU ZA VIATU
    KANDO YA KABURI, NA KIBAJAJI
    !!!!!




No comments:

Post a Comment