- 
 jamani hakuna mtu wa kumpamedali huyu jamaaa!!! Kuna jamaa alikuwa anaishi karibu Kuna jamaa alikuwa anaishi karibu
 na makaburi. Basi akajigundulia njia
 ya kupata usafiri bila ya kulipa...
 Akawa kila akikodi bodaboda au
 bajaji mida ya jioni jioni alikuwa
 anaomba kuachwa makaburini.....
 Katikati ya safari akawa anajipaka
 poda usoni na kuweka pamba
 kwenye pua zake then wakati wa
 kushuka anaongea kwa kubana
 pua...
 . 
 "Nimefika home unanidai shilingi
 ngapi?!?"
 .Madereva wote wa bodaboda na
 bajaji walikuwa wanatoka nduki....
 Siku moja akafanya mchezo huo
 kwa dereva mmoja wa bodaboda
 mtoto wa TANDALE kapinda
 mbaya!!! Walipofika mwisho wa
 safari dereva wa bodaboda
 hakutishika na mapoda wala pamba
 puani....
 Akakomaa anataka nauli 
 yake!!!!
 JAMAA: "Ooooooky!!!! Twende
 kwenye kaburi langu nikakupe
 chako....!!!"
 Dereva ya boda boda kumbe
 alikuwa ameshaskia story za jamaa
 so akakomaa na kumwambia...
 BAJAJI: "Haina noma mtu wangu....
 Twende ukanipe changu nsepe...."
 maana hasira nilizonazo naweza kukulamba wewe na mapoda yako 
 Walipofika kaburi fulani, jamaa
 akagonga msalaba....
 JAMAA: "Wakulu, wakulu fungueni
 nipeni alfu nane huyu jamaa
 ananidai nauli......!!!!"
 Ghafla mkono mrefu wenye
 manyoya ukatoka kaburini ukiwa
 umeshika noti ya msimbazi....
 DAAAH, NDUGU ZANGU ASUBUHI 
 KULIKUTWA PEA MBILI TUU ZA VIATU
 KANDO YA KABURI, NA KIBAJAJI
 !!!!!
 
Thursday, 18 July 2013
mtoto wa TANDALE
Subscribe to:
Post Comments (Atom)

No comments:
Post a Comment