Vijana wengi ambao wanapendana leo
 
 Vijana wengi ambao wanapendana leo
 
 Vijana wengi ambao wanapendana leo
Vijana wengi ambao wanapendana leo
 mapenzi yao hayadumu kiasi cha
 kubatishwa jina la utamu wa bazoka.
 Lakini yote hii inatokana na ukweli
 kwamba elimu ya mapenzi ambayo ni
 muhimu kwa binadamu haitolewi ipasavyo.
 Ipo zana potofu kwamba kumfundisha
 motto mapenzi ni kumharibu, jambo
 ambalo si kweli bali inategemea mtoto
 huyo anafundishwa nini na kwa wakati
 gani. Lakini cha kushangaza zaidi hata watu wazima ambao ni wadau wa
 mapenzi hawayajui, matokeo yake
 wanajiingiza kwenye uhusiano wakiwa
 bumbumbu na hivyo kuteshwa na
 changamoto za mepenzi.
 Leo tutajifunza kwa undani sifa kumi za mpenzi bora ili tuweze kuwatambua
 wapenzi wetu kabla ya kuwapa mioyo na
 utu wetu. Sifa hizo hizi zifuatazo.
 1. Mpenzi wa kweli ni yule ambaye
 hatangoja kujua nini unahitaji yaani hana
 sababu ya kusubiri kuombwa ndiyo atoe msaada.
 2. Ni yule atakayejua wakati gani huna
 furaha au una furaha na atakuwa na
 wewe kwa hali zote mbili .
 3. Ni yule atayekuwa tayari kukusikiliza
 kwa kile utakachosema, hatojali umeongea baya au zuri .
 4. Atakuwa na wewe wakati wa shida na
 raha. Hatakuacha mtu wa kuvizia vizia na
 kujisogeza wakati ukiwa na raha.
 5. Mpenzi wa kweli atakuheshimu na
 hatopenda kuwa nyuma na kukuacha bila msaada .
 6.Atakupenda kwa moyo wake wote na
 wala si kwa ajili ya shinikizo fulani (pesa
 au mali)
 7.Mpenzi wa kweli ni yule
 atakayeonyesha kuthamini nafasi yako kama rafiki au mpenzi mbele ya wengine
 8. Kwenye ukweli mpenzi mzuri atasema
 bila kukuficha na atapenda kukuonyesha
 mifano ya namna ya kuwa mkweli na
 mwaminifu.
 9. Mpenzi wa kweli ni yule anayejiamini, asiyeyumba katika maamuzi hata kama
 atalazimika kufanya maamuzi magumu .
 10.Atakuwa tayari kuvumilia, hatakuwa
 mwepesi wa hasira wala kutumia lugha
 chafu na ubabe.
 
 
 
          
      
 
  
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment