
KILIMANJARO 

AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA
KUGHUSI SAINI YA PINDA


 
 MFANYABIASHARA Amadi Ally Popi (35), jana alifikishwa mbele ya Hakimu 
Mkazi wa MAhakama ya Hakimu Mkazi Kisutu – Dar es Salaam, Waliarwande 
Lema akishtakiwa kwa makosa mawili likiwemo la kughushi barua 
inayoonyesha imeandikwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.
 
 Inspekta
 wa Polisi Hamis Said, aliiambia Mahakama kuwa tarehe na siku 
isiyofahamika ndani ya jiji la Dar es Salaam, kwa nia ya kudanganya 
Amadi Ally Popi alighushi barua yenye kumbukumbu Na. DA21/3078/01A/142 
ya Desemba 3, 2012 akijaribu kuonyesha kuwa barua hiyo ni halali na 
ilikuwa imeandikwa na kusainiwa na Waziri Mkuu, Pinda.
 
 Alidai shtaka lingine ni kuwa tarehe na siku isiyofahamika ndani ya 
jiji la Dar es Salaam, bila ya kuwa na mamlaka yoyote alitengeneza barua
 hiyo na kuisani na kisha alimpatia Islamu Mohammed Mtila akijaribu 
kuonyesha barua hiyo imetoka katika Ofisi ya Waziri Mkuu na imesainiwa 
na Pinda.
 
 Mshtakiwa alikana tuhuma hizo na kupelekwa rumande 
hadi tarehe 5-Septemba kesi hiyo itapotajwa tena. Hii ilikuwa ni baada 
ya mstakiwa kushindwa kutimiza masharti ya dhamana ya kuwa na wadhamini 
wawili wanaofanya kazi serikalini au kwenye taasisi zinazofahamika 
watakaosaini bondi ya sh milioni 10.
|  | 
| MBUGA ZA WANYAMA.. Tz | 
No comments:
Post a Comment