TAHADHARI: FEDHA NI HATARI KWA AFYA YAKO 
 

 

 
 
 
Fedha ni hatari kwa afya ya binadamu kwani huweza kusababisha madhara makubwa.
 Katika uchunguzi, ilibainika kuwa fedha za noti na zile za sarafu 
huweza kukusanya na kusambaza vimelea vya magonjwa hatari kutoka kwa mtu
 mmoja kwenda kwa mwingine.
 
 
Mtaalam wa magonjwa mbalimbali, Dk. Richard Marise, ametanabahisha 
kwamba tafiti mbalimbali duniani zimeripoti kuhusu vimelea vinavyoweza 
kusafirishwa kupitia fedha ambavyo ni Staphylococcus Aureus, 
Escherichiacoli,Fecal Bacteria na sumu nyingine.
 “Tafiti nyingi 
zilizofanywa katika nchi zilizoendelea, zimegundua kuwa vimelea 
hatarishi kwenye fedha hasa za noti ambapo vingi hutokana na uchafu 
utokao kwa mwanadamu mwenyewe kwa mfano; kinyesi, mkojo na jasho.
 
 “Vimelea hivyo kwa pamoja husababisha magonjwa kama boils (magonjwa ya 
ngozi) pneumonia, toxic shock syndrome (homa za sumu mwilini), diarrhea 
(kuharisha), gum diseases (magonjwa ya fizi), homa za vipindi na 
meningitis (uvumbi wa bongo) ambao kama hakuna matibabu huweza 
kusababisha kifo,” 
alisema Dk. Richard.
 
 Akifafanua jinsi fedha 
zinavyoweza kusafirisha magonjwa, daktari huyo alisema fedha huweza 
kushikwa na mtu asiyeosha mikono yake kwa maji safi na sabuni baada ya 
kutoka kujisaidia, kisha hela hiyo huweza kutua mikononi mwa mtu 
mwingine ambaye huacha jasho lake na kuongeza vimelea vya magonjwa 
mengine juu yake.
 Mzunguko huo unaweza ukawa mkubwa kufikia hatua ya
 vimelea kusambaa kwa mamilioni ya watu hivyo kuifanya jamii kuwa katika
 hatari zaidi ya maambukizi ya ugonjwa husika.
 
 Dk. Richard 
alikazia kuwa
 “maambukizi hutokea kama mtu aliyeshika hela hizo atagusa 
sehemu zenye unyevunyevu kwenye mwili wake kwa mfano jicho, mdomo na pua
 ambapo vimelea hivyo vitapata nafasi ya kuingia ndani ya mwili.”
 
 Katika mazingira ya kawaida, fedha zenyewe huhifadhiwa katika mazingira
 hatarishi ambapo kuna mifano ya watu kuhifadhi fedha ndani ya nguo za 
ndani au kwenye matiti (akina mama zaidi). Fedha pia huweza kudondoka 
kwenye uchafu wa aina mbalimbali na kuokotwa kisha ikatumika tena. 
Ukiachilia mbali kubeba vimelea vya magonjwa, fedha zinaweza kubeba sumu
 na madawa ya kulevya juu yake ikiwa itapitia kwenye mikono ya mtu 
aliyeshika vitu hivyo.
 
 “Ni vyema ukatumia fedha kwa uangalifu, 
 usiweke hela mdomoni na ukumbuke kuosha mikono yako kila mara kwa maji 
na sabuni ili kujikinga na maambukizi,” 
 alitahadharisha Dk. Richard.
 
No comments:
Post a Comment