JAPANI YAWEKEZA TANZANIA...
.MRADI WA PIKIPIKI
Dar es Salaam. Serikali ya Japan imesema ina mpango kabambe wa kukuza uchumi wa Tanzania, ikiwa ni pamoja na kampuni kubwa duniani za Honda na Panasonic kujenga viwanda vitakavyokuwa matawi yake hapa nchini.

 Uamuzi na msimamo wa Japan umetangazwa jana jijini
 Dar es Salaam na Waziri wa Uchumi, Biashara na Viwanda wa nchi hiyo, 
Toshimistu Motegi alipokutana na kufanya mazungumzo na Rais Jakaya 
Kikwete, Ikulu.
Uamuzi na msimamo wa Japan umetangazwa jana jijini
 Dar es Salaam na Waziri wa Uchumi, Biashara na Viwanda wa nchi hiyo, 
Toshimistu Motegi alipokutana na kufanya mazungumzo na Rais Jakaya 
Kikwete, Ikulu.
Taarifa ya Ikulu iliyosambazwa na Kurugenzi ya 
Mawasiliano ya Rais, ilimnukuu Motegi akisema: “Kwa kuanzia kampuni 
mbili za Honda na Panasonic zimekubali kujenga viwanda nchini, kimoja 
kwa ajili ya kutengeneza pikipiki za Honda na kingine kwa ajili ya 
kutengeneza vifaa vya umeme.”
Akaweka msisitizo: “Huu ni mwanzo tu Mheshimiwa 
Rais (Kikwete) kwa sababu kama nilivyosema kuwa tunataka Tanzania kuwa 
nchi ya mfano ya uwekezaji wa Japan katika eneo hili la dunia, na namna 
hiyo kwa pamoja tutakuwa tumeshirikiana katika kuongeza ajira kwa 
wananchi wa Tanzania.”
Waziri huyo pia alisema kuwa baadhi ya kampuni za 
Japan zina mipango ya kuwekeza katika kilimo, na hasa kilimo cha pamba 
na kuanzisha viwanda vya nguo hapahapa nchini.
Motegi alisema mikakakati mingine ya kuisaidia 
Tanzania ni pamoja na kushiriki uboreshaji wa Reli ya Kati, kusaidia 
kupanua na kuboresha Bandari ya Dar Es Salaam.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo ya Ikulu, mkakati huo wa Japan unatokana na ziara ya Rais Kikwete nchini humo, Juni mwaka huu.
“Japan imeamua kuanzisha ushirikiano mkubwa zaidi 
na Tanzania ambako nchi hiyo itaifanya Tanzania kuwa nchi lengwa ya 
kuwekeza na kuifanya kuwa kitovu cha biashara na uwekezaji katika 
Afrika,” inasema sehemu ya taarifa hiyo.
Taarifa hiyo iliweka wazi kuwa Waziri Motegi 
alimweleza Rais Kikwete kuwa ametumwa na Waziri Mkuu Abe, kufuatilia 
mazungumzo kati yao na kutangaza rasmi kuwa Japan imeiteua Tanzania kuwa
 nchi lengwa na kitovu cha uwekezaji Afrika Mashariki na Afrika kwa 
jumla.
Waziri Motegi amesema kuwa katika kufanikisha 
mkakati huo aliandamana na kundi la wafanyabiashara wa Japan ambao 
wanaendelea kufanya mazungumzo na wafanyabiashara wa Tanzania, kuona 
jinsi gani wanavyoweza kusaidiana katika kuwekeza katika uchumi wa 
Tanzania.
No comments:
Post a Comment