|  | 
| Tembo wa Tanzania | 
 | 
 | 
 | 
 | 
|  |  | 
| Jicho la Africa | 
|  | 
| Mapambano D.R.Congo | 
|  | 
| Wanajeshi -DRC | 
Vikosi vya serikali ya Congo na wapiganaji waasi wamepambana
Daktari mmoja aliyekuwa mstari wa mbele katika mapigano hayo amesema 
huduma za afya zimepata changamoto kubwa kutokana na majeruhi wengi. 
Mapigano baina ya jeshi la serikali na kundi la waasi wa M23 yalidumu 
usiku kucha kuanzia Jumamosi hadi Jumapili huko Mujoga takriban kilomita
 17 kaskazini mwa Goma.
Daktari Isaac Warwanamiza ameiambia Sauti ya Amerika kwa njia ya simu 
alikuwa hospitali pamoja na Watanzania walioko katika jeshi la Umoja wa 
Mataifa wakisubiri kwenda mstari wa mbele na kwamba  wote waliomzunguuka
 waliuawa na wengine wengi ni majeruhi.Alisema kufikia Jumapili asubuhi 
watu 82 walikuwa wameuawa.
Wakati, huo, huo Marekani imesema imeshtushwa na ghasia zinazoendelea 
baina ya kundi la M23 na jeshi la FARDC mashariki mwa Congo. Katika 
taarifa iliyotolewa Jumapili jioni na wizara ya mambo ya nje ya Marekani
 ililaani hatua ya waasi wa M23 ya kusababisha majeruhi ya raia na 
kushambulia tume ya walinda amani wa Umoja wa Mataifa MONUSCO na 
kupelekea raia wengi kutoroka manyumbani mwao.
 
 vikali katika siku ya tano ya mapigano mashariki mwa mji wa Goma.
|  | 
| Twiga wa Tanzania | 
 
No comments:
Post a Comment