|  | 
| Tembo | 
|  | 
| WAZIRI WA MABO YA NDANI | 
|  | 
| ASKARI... POLICE | 
Majukumu waliyoshindwa kuyasimamia  maofisa hao 
yalisababisha askari  10 wa vyeo vya chini kushindwa kuwajibika ipasavyo
 na kufanya mambo kinyume na majukumu yao, hivyo kusababisha saba kati 
yao kufukuzwa kazi, mmoja kusimamishwa na wawili kupewa onyo kali.
Ilinishangaza kwa kuwa Dk Nchimbi alisahau kuwa 
mara kadhaa wananchi na wanaharakati wamekuwa wakiwataka baadhi ya 
mawaziri wa serikali ya Rais Jakaya Kikwete akiwamo Dk Nchimbi mwenyewe,
 wajiuzulu kutokana na kushindwa kusimamia majukumu yao,  tena kwa 
uzembe au makosa ambayo hawajayafanya wao bali yamefanywa na watu walio 
chini yao.
Tukio la kuuawa kwa aliyekuwa mwandishi wa habari 
wa Channel Ten, Daudi Mwangosi  katikati ya mikono ya polisi pamoja na 
matukio ya wananchi kuuawa kwa kupigwa risasi  mkoani Morogoro, Arusha, 
Tabora nani alivuliwa madaraka, wakati maofisa wa jeshi hilo walikuwapo 
maeneo ya tukio na inawezekana walishuhudia kinachoendelea?
Wiki mbili zilizopita askari ‘feki’ wa usalama 
barabarani mwenye cheo cha sajini alikamatwa akiwa katika majukumu kama 
yanayofanywa na askari halisi wa kikosi hicho, lakini hadi sasa 
hatujasikia kuchukuliwa hatua za kinidhamu dhidi ya ofisa yeyote wa 
kikosi hicho.
Inawezekana kabisa wanaohusika katika matukio ya  
uhalifu na utapeli yanayoidhalilisha  polisi na nchi kwa ujumla ni 
maofisa wa ngazi za juu ambao wanawatumia askari wa vyeo vya chini, 
hivyo nao wanatakiwa kuchukuliwa hatua stahiki, siyo kuvuliwa madaraka 
tu.
Huenda jeshi limepwaya kiutendaji, limeelemewa na 
matukio mabaya, baadhi ya askari wake wamechafuka, hivyo wanaleta picha 
mbaya kwa jeshi zima?
Baada ya kauli ile ya Dk Nchimbi, nilijiuliza 
maswali mengi kichwani, hivi polisi wakikosea wanachunguzwa na nani, au 
iundwe tume huru kuwachunguza maana inaonekana wazi kuwa sasa 
limeshindwa kujichunguza lenyewe  kama ambavyo imekuwa ikitokea hata kwa
 mambo ambayo wanatuhumiwa wao.
Nasema hivi baada ya kutafakari utitiri wa matukio
 ya uhalifu nchini ukiwamo ujambazi, utekaji, uteswaji na kushambuliwa 
kwa watu na hata mauaji.
Jeshi limeshindwa kukabiliana  na vitendo hivyo, 
ndiyo maana wananchi wamefikia hatua ya kulaumu na kulalamika kuwa kasi 
ya polisi imeshuka kiasi cha kushindwa kuwabaini wahalifu.
Hivi sasa matukio yanayovihusu vyama vya upinzani 
ndiyo yanayopewa kipaumbele, ikiwa ni pamoja na upelelezi kukamilika kwa
 wakati na watuhumiwa kukamatwa usiku wa manane, kusafirishwa kwa 
helikopta kupelekwa mahakamni tena kwa mbwembwe za hali ya juu.
Mpaka leo zimebaki stori tu kwa baadhi ya matukio 
likiwamo lile la Dk Stephen Ulimboka, polisi wanataka ushahidi gani 
kuthibitisha makosa yaliyofanywa na askari wake, matukio ambayo picha 
zake zipo tena hadharani tu katika vyombo vya habari.
Sitaki kuzungumzia kesi zilizopo mahakamni, lakini zipo ambazo 
ushahidi wake ulifanyika kwa siku chache tu, lakini yale matukio 
yaliyowasababishia watu ulemavu, mauti mpaka leo yamesokomezwa chini ya 
kapeti.
Wiki hii polisi saba ‘feki’  walikamatwa wakiwa na
 sare za jeshi hilo, tena wakiwa doria huku mmoja akiwa na cheo cha meja
 na walikuwa na redio ya mawasiliano pamoja na  bastola, jambo ambalo 
linaonyesha wazi kuwa kuna kitu kinaendelea ndani ya jeshi hilo.
Huenda watu wa namna hii wakawa na mtandao wao 
ndani ya jeshi hilo, mtandao ambao unawalinda, unawapatia sare za 
polisi, bastola na hata kuweka vigingi ili wasikamatwe na polisi 
wanaofuata maadili ya kazi yao.
Ndiyo maana nikasema kuwa kuwafukuza kazi askari 
wa vyeo vya chini siyo suluhisho, aliyeshiriki wizi na ambaye ameshindwa
 kusimamia majukumu yake mpaka wizi ukatokea wote wanatakiwa kufukuzwa 
kazi ili iwe fundisho kwa wengine, nani anayejua pengine nao walihusika 
kwa namna moja au nyingine.
Kwa mtindo huu siyo ajabu tukasikia yule Msaidizi 
Mwandamizi wa Polisi aliyekuwa anasimamia ajira katika jeshi hilo, 
Renatus Chalamila, ambaye alipewa likizo baada ya kutajwa mara nyingi 
kuhusika kuwatoza fedha vijana walioomba ajira za uaskari, akavuliwa 
madaraka yake kama ilivyotokewa kwa wale maofisa wanne.

No comments:
Post a Comment