WAZEE wetu walikuwa na sababu
 
 Eiyer, WAZEE wetu walikuwa na sababu ya kuzuia wachumba kukutana kimwili kabla ya ndoa…! 
 
 
   
    
|  | 
| mahusiani | 
     

Nimesoma mada ya rafiki yangu Eiyer
 kuhusiana na suala la wanandoa kukutana kimwili kabla ya kufunga ndoa 
ili kufahamiana zaidi. Lengo kama alivyoeleza rafiki yangu huyu ni  
kuepuka mitafaruku inayoweza kutokea baada ya kuingia katika ndoa na 
kukutana na hali ambayo haikutarajiwa. Ukitaka kujikumbusha kuhusu mada 
hiyo bofya hapa:
Yes,i'm goin to marry you,but before that i just wanna make sure of something...
 Eiyer
 ametoa mifano kadhaa ambayo siwezi kuipinga, lakini lengo langu hapa ni
 kuweka angalizo kuhusiana na suala zima la kukutana kimwili kwa wapenzi
 kabla ya ndoa ili wanaofanya hivyo waweze kujua athari za kufanya jambo
 hilo ni zipi?
Ni kweli kwamba, siku hizi vijana wengi huamini kuwa, baada ya kukutana 
kimwili, ndipo wanapoweza kudai  kwamba, wamewafahamu wapenzi wao vizuri
 na kwamba kukutana kimwili ndiyo mapenzi au kupendana kwenyewe. 
Wanapokutana kimwili  na kuvutiwa na tendo la kujamiiana, huamini kabisa
 kwamba, uhusiano nao utakuwa mzuri. Kwao, tendo la kujamiiana ndiyo 
kipimo cha uimara wa uhusiano wao.
 
Baada ya kufanya mapenzi, wapenzi huamini  kwamba, sasa wanaweza 
kujitolea  kwenye uhusiano huo na kwamba, wanaweza kuwa na nguvu nao. 
Suala hili, wataalamu huliita  mtego wa kimapenzi. Huitwa hivyo  kwa 
sbabu huwafanya wapenzi kutoangalia  sifa  nyingine  na badala yake 
kuweka nguvu kwenye mwili, yaani tendo la kujamiiana.
Upofu hutokea kutokana na kuzalishwa  kwa kemikali nyingi mwilini, zenye
 kumfanya mtu asiweze kujiuliza kuhusu maeneo mengine ya kimaisha ya 
binadamu, zaidi ya mwili. Kinachotokea ni miili kuvutwa na wale tunaodai
 tunawapenda kwa kuzalisha homoni inayofahamika kama phenylethylamine au PEA kwa kifupi.
Kemikali au homoni hii pamoja na nyingine kama vile dopamine na norepinephrine (ambazo huchochea hali ya kimwili) na testosterone
 (ambayo huongeza hamu ya kujamiiana), huzalishwa baada tu ya kukutana 
kimwili. Baada ya kuzalishwa kwa homoni hizi, akili ya mtu huona mwili  
tu, yaani mapenzi na siyo sifa nyingine.
Hapa ndipo ambapo, mtu anajikuta  hawezi kujizuia kukutana tena kimwili 
 na mpenzi wake, mara baada ya kukutana naye mara moja. Baada ya kufanya
 mapenzi na kufika kileleni, huzalishwa homoni iitwayo oxytocin
 (ambayo huhusika na mihemko), homoni hii humfanya mtu kujikuta anapenda
 kuwa karibu  na kujifunganisha na mtu aliyefanya naye mapenzi. Naweza 
kusema ukaribu kwa wapenzi wawili huongezeka na unakuwa ni ukaribu wa 
mwili zaidi.
Kuzalishwa kwa homoni hizi, ni jambo ambalo mtu hawezi kulizuia  na huwa
 linakuja kwa nguvu sana, kiasi kwamba, mtu huwa kama amepoteza ufahamu 
wa maeneo mengine  ya kimaisha isipokuwa mapenzi tu.  Wale waliowahi 
kuwa na uhusiano wa kimapenzi kabla ya ndoa au wale wanaotoka nje ya 
ndoa zao kwa kuvutwa  kimwili  na wapenzi  wengine wanajua inavyokuwa.
Lakini homoni hizi, hatimaye huanza kupungua na mtu huanza kuhisi 
kwamba, alikosea. Haoni tena au kuhisi kama ilivyokuwa awali. Sasa haoni
 kuwa mpenzi wake ni mzuri au anayefaa kama alivyokuwa  anaona awali. 
Kwa sababu, homoni zile zimeshuka sana, mwili unakuwa hauna maana tena. 
Kwa bahati mbaya kile kilichokuwa kinaitwa upendo kilikuwa kimefungiwa 
kwenye mwili na homoni hizo ambazo sasa hazipo. Hivyo, wapenzi hawana 
tena cha kushika ambacho, wataweza kukiita mapenzi.
Naamini sasa unajua ni kwa nini tangu kale kabisa suala la wachumba  
kukutana kimwili  kabla ya ndoa lilikuwa linapingwa sana na wazee wetu. 
Ni kwamba, watu wanapokutana kimwili , uwezo wa kukaguana tabia unakuwa 
umefungwa kutokana na kufumuka kwa homini hizi ambazo, hubadili hali ya 
mtu na hisia zake kwa ujumla.
Hebu jiulize, ni kwa nini mapenzi yanayoanza kwa moto sana,huzimika 
haraka au kwa kishindo sana? Ni kwa sababu yamejengwa juu ya msingi 
usioaminika, yaani kutokana na mihemko ya kimapenzi! Penzi linalokuwa 
polepole na lisilotanguliza kukutana kimwili ndilo lenye kushika, kwani 
halina msingi wa mwili…..
 
 
 
 
 
          
      
 
  
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment